Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 34:31-37 Biblia Habari Njema (BHN)

31. “Tuseme mtu amemwambia Mungu,‘Nimekosa, sitatenda dhambi tena.

32. Nioneshe makosa nisiyoweza kuyaonakama nimetenda mabaya sitayarudia tena.’

33. Je, Mungu atapaswa kumwadhibu kama uonavyo wewe?Wewe ndiwe unayeamua, sio mimi.Basi, sema unachofikiri wewe.

34. Mtu yeyote mwenye akili,na kila mwenye hekima anayenisikiliza atasema:

35. ‘Yobu anaongea bila kutumia akili,maneno yake hayana maana.’

36. Laiti Yobu angechunguzwa mpaka mwisho,kwa maana anajibu kama watu waovu.

37. Huongeza uasi juu ya dhambi zake;anaeneza mashaka kati yetu,na kuzidisha maneno yake dhidi ya Mungu.”

Kusoma sura kamili Yobu 34