20. Kufumba na kufumbua hao wamekufa;hutikiswa usiku na kuaga dunia;nao wenye nguvu hufutiliwa mbali bila kutumia nguvu za mtu.
21. “Macho ya Mungu huchunguza mienendo ya watu;yeye huziona hatua zao zote.
22. Hakuna weusi wala giza neneambamo watenda maovu waweza kujificha.