Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 34:14-20 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Kama Mungu angejifikiria tu yeye mwenyewe,akiondoa pumzi yake ya uhai duniani,

15. viumbe vyote vingeangamia kabisa,naye binadamu angerudi mavumbini.

16. “Kama una akili sikiliza;sikiliza ninachokuambia.

17. Je, anayetawala ulimwengu kwa sheria zake anachukia haki?Je, utathubutu kumhukumu mwadilifu na mwenye nguvu?

18. Amwambiaye mfalme, ‘Wewe ni takataka!’Na watu mashuhuri, ‘Nyinyi ni waovu!’

19. Yeye hawapendelei wakuu,wala kuwajali matajiri kuliko maskini,maana wote hao ni kazi ya mikono yake.

20. Kufumba na kufumbua hao wamekufa;hutikiswa usiku na kuaga dunia;nao wenye nguvu hufutiliwa mbali bila kutumia nguvu za mtu.

Kusoma sura kamili Yobu 34