Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 34:1-11 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Elihu akaendelea kusema:

2. “Sikilizeni maneno yangu enyi wenye hekima,nitegeeni masikio yenu, nyinyi wenye ujuzi.

3. Sikio huyapima maneno,kama vile ulimi uonjavyo chakula.

4. Basi, na tuchague lililo sawa,tuamue miongoni mwetu lililo jema.

5. Basi, Yobu ametamka: ‘Mimi Yobu sina hatia,Mungu ameniondolea haki yangu.

6. Ingawa sina hatia naonekana kuwa mwongo;kidonda changu hakiponyeki ingawa sina kosa.’

7. Ni nani aliye kama Yobuambaye kwake ubaradhuli ni kama kunywa maji?

8. Huandamana na watenda maovuhutembea na watu waovu.

9. Maana amesema, ‘Mtu hapati faida yoyote,kujisumbua kumpendeza Mungu.’

10. “Kwa hiyo nisikilizeni, enyi wenye ujuzi.Mungu kamwe hawezi kufanya uovu;Mungu Mwenye Nguvu hawezi kufanya kosa.

11. Mungu atamlipa mtu kadiri ya matendo yake,atamlipiza kulingana na mwenendo wake.

Kusoma sura kamili Yobu 34