Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 33:6-20 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Wewe na mimi ni sawa mbele ya Mungu;mimi pia niliumbwa kwa sehemu ya udongo.

7. Kwa hiyo huna sababu ya kuniogopa;maneno yangu mazito hayatakulemea.

8. Kweli umesema, nami nikasikia;nimeyasikia yote uliyosema.

9. Wewe umesema, u safi na wala huna kosa,u safi kabisa na huna hatia;

10. umesema kwamba Mungu anakutafutia kisa,na kukuona kama adui yake.

11. Anakufunga miguu minyororo,na kuchunguza hatua zako zote.

12. “Lakini Yobu, nakuambia hapo umekosea.Mungu ni mkuu kuliko binadamu.

13. Kwa nini unashindana naye,ukisema hatajibu swali lako moja?

14. Mungu anaposema hutumia njia moja,au njia nyingine lakini mtu hatambui.

15. Mungu huongea na watu katika ndoto na maono,wakati usingizi mzito unapowavamia,

16. wanaposinzia vitandani mwao.Hapo huwafungulia watu masikio yao;huwatia hofu kwa maonyo yake,

17. wapate kuachana na matendo yao mabaya,na kuvunjilia mbali kiburi chao.

18. Hivyo humkinga mtu asiangamie shimoni,maisha yake yasiangamie kwa upanga.

19. “Mungu humrudi mtu kwa maumivu yamwekayo kitandani,maumivu hushika viungo vyake bila kukoma;

20. naye hupoteza hamu yote ya chakula,hata chakula kizuri humtia kinyaa.

Kusoma sura kamili Yobu 33