Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 33:17-24 Biblia Habari Njema (BHN)

17. wapate kuachana na matendo yao mabaya,na kuvunjilia mbali kiburi chao.

18. Hivyo humkinga mtu asiangamie shimoni,maisha yake yasiangamie kwa upanga.

19. “Mungu humrudi mtu kwa maumivu yamwekayo kitandani,maumivu hushika viungo vyake bila kukoma;

20. naye hupoteza hamu yote ya chakula,hata chakula kizuri humtia kinyaa.

21. Mwili wake hukonda hata asitambuliwe,na mifupa yake iliyofichika ikatokeza nje.

22. Yuko karibu sana kuingia kaburini,na maisha yake karibu na wale waletao kifo.

23. Lakini malaika akiwapo karibu naye,mmoja kati ya maelfu ya watetezi wa Mungu,ili kumwonesha lililo jema la kufanya,

24. akamwonea huruma na kumwambia Mungu;‘Mwokoe asiingie Shimoni,ninayo fidia kwa ajili yake.’

Kusoma sura kamili Yobu 33