Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 30:21-27 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Umegeuka kuwa mkatili kwangu,wanitesa kwa mkono wako wenye nguvu.

22. Wanitupa katika upepo na kunipeperusha;wanisukasuka huku na huko katika dhoruba kali.

23. Naam! Najua utanipeleka tu kifoni,mahali watakapokutana wote waishio.

24. “Je, mtu akikumbwa na maangamizi hainui mkono?Je, mtu akiwa taabuni haombi msaada

25. Je, sikuwalilia wale waliokuwa na taabu?Je, sikuona uchungu kwa ajili ya maskini?

26. Lakini nilipotazamia mema, mabaya yalinipata,nilipongojea mwanga, giza lilikuja.

27. Moyo wangu wahangaika wala hautulii kamwe;siku za mateso zimekumbana nami.

Kusoma sura kamili Yobu 30