Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 30:16-23 Biblia Habari Njema (BHN)

16. “Sasa sina nguvu yoyote nafsini mwangu;siku za mateso zimenikumba.

17. Usiku mifupa yangu yote huuma,maumivu yanayonitafuna hayapoi.

18. Mungu amenikaba kwa mavazi yangu,amenibana kama ukosi wa shati langu.

19. Amenibwaga matopeni;nimekuwa kama majivu na mavumbi.

20. Nakulilia, lakini hunijibu,nasimama kuomba lakini hunisikilizi.

21. Umegeuka kuwa mkatili kwangu,wanitesa kwa mkono wako wenye nguvu.

22. Wanitupa katika upepo na kunipeperusha;wanisukasuka huku na huko katika dhoruba kali.

23. Naam! Najua utanipeleka tu kifoni,mahali watakapokutana wote waishio.

Kusoma sura kamili Yobu 30