16. “Sasa sina nguvu yoyote nafsini mwangu;siku za mateso zimenikumba.
17. Usiku mifupa yangu yote huuma,maumivu yanayonitafuna hayapoi.
18. Mungu amenikaba kwa mavazi yangu,amenibana kama ukosi wa shati langu.
19. Amenibwaga matopeni;nimekuwa kama majivu na mavumbi.
20. Nakulilia, lakini hunijibu,nasimama kuomba lakini hunisikilizi.
21. Umegeuka kuwa mkatili kwangu,wanitesa kwa mkono wako wenye nguvu.
22. Wanitupa katika upepo na kunipeperusha;wanisukasuka huku na huko katika dhoruba kali.
23. Naam! Najua utanipeleka tu kifoni,mahali watakapokutana wote waishio.