Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 30:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Lakini sasa watu wananidhihaki,tena watu walio wadogo kuliko mimi;watu ambao baba zao niliwaona hawafaihata kuwaangalia mbwa wangu wakilinda kondoo.

2. Ningepata faida gani mikononi mwao,watu ambao nguvu zao zilikuwa zimewaishia?

3. Katika ufukara na njaa kaliwalitafutatafuta cha kutafuna nyikanisehemu tupu zisizokuwa na chakula.

4. Walichuma mimea jangwani na majani msituni wakala,walikula hata mizizi ya mti wa mfagio.

5. Walifukuzwa mbali na watu,watu waliwapigia kelele kama wezi.

6. Iliwapasa kutafuta usalama mapangoni,kwenye mashimo ardhini na miambani.

7. Huko vichakani walilia kama wanyama,walikusanyika pamoja chini ya upupu.

8. Walikuwa wapumbavu wakuu na mabaradhuliambao walilazimika kufukuzwa nchini kwa kiboko.

9. “Na sasa wamenitungia wimbo wa kunizomea,nimekuwa kitu cha dhihaka kwao.

10. Wananichukia na kuniepa;wakiniona tu wanatema mate.

Kusoma sura kamili Yobu 30