Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 29:8-13 Biblia Habari Njema (BHN)

8. vijana waliponiona walisimama kando,na wazee walisimama wima kwa heshima.

9. Wakuu waliponiona waliacha kuzungumzawaliweka mikono juu ya midomo kuwataka watu wakae kimya.

10. Sauti za waheshimiwa zilinyamazishwa,na vinywa vyao vikafumbwa.

11. Kila aliyesikia habari zangu alinitakia herina aliponiona, alikubali habari hizo kuwa kweli:

12. Nilimwokoa maskini aliyenililia msaada,kadhalika na yatima asiyekuwa na wa kumsaidia.

13. Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka,niliwafanya wajane waone tena furaha moyoni.

Kusoma sura kamili Yobu 29