Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 29:20-25 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Napata fahari mpya daima,na nguvu zangu tayari kama mshale na upinde.

21. “Wakati huo watu walinisikiliza na kungoja,walikaa kimya kungojea shauri langu.

22. Nilipomaliza kusema hawakuwa na cha kuongeza,maneno yangu yaliwakolea kama matone ya mvua.

23. Watu waliningojea kama wangojeavyo mvua,walikuwa kama watu wanaotazamia msimu wa vuli.

24. Walipokata tamaa niliwaonesha uso wa furaha,uchangamfu wa uso wangu wakaungangania.

25. Niliwatangulia kuwaongoza, nikawaonesha njia;nilikuwa kwao kama mfalme kati ya majeshi yake;kama mtu anayewafariji wenye msiba.

Kusoma sura kamili Yobu 29