Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 29:10-14 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Sauti za waheshimiwa zilinyamazishwa,na vinywa vyao vikafumbwa.

11. Kila aliyesikia habari zangu alinitakia herina aliponiona, alikubali habari hizo kuwa kweli:

12. Nilimwokoa maskini aliyenililia msaada,kadhalika na yatima asiyekuwa na wa kumsaidia.

13. Waliokuwa karibu kuangamia walinitakia baraka,niliwafanya wajane waone tena furaha moyoni.

14. Uadilifu ulikuwa vazi langu;kutenda haki kulikuwa kama joho na kilemba changu.

Kusoma sura kamili Yobu 29