Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 28:6-12 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Katika mawe yake ndimo vilimo vito vya rangi ya samawatina udongo wake una vumbi la dhahabu.

7. “Njia za kwenda kwenye migodi hiyohakuna ndege mla nyama azijuaye;na wala jicho la tai halijaiona.

8. Wanyama waendao kwa madaha hawajazikanyagawala simba hawajawahi kuzipitia.

9. Binadamu huchimbua miamba migumu kabisa,huichimbua milima na kuiondolea mbali.

10. Hupasua mifereji kati ya majabali,na jicho lake huona vito vya thamani.

11. Huziba chemchemi zisitiririke,na kufichua vitu vilivyofichika.

12. “Lakini hekima itapatikana wapi?Ni mahali gani panapopatikana maarifa?

Kusoma sura kamili Yobu 28