Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 24:9-13 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Wapo na wanaowanyakua watoto yatima vifuani mwa mama yao.Wengine huwaweka rehani watoto wa maskini.

10. Watoto hao hufanywa waende uchi bila nguo,wakivuna ngano huku njaa imewabana,

11. wakiwatengenezea waovu mafuta yao,au kukamua divai bila hata kuionja.

12. Kutoka mjini kilio cha wanaokufa chasikika,na walioumizwa hupaza sauti kuomba msaada;lakini Mungu hasikilizi kabisa sala zao.

13. “Wapo wengine waovu wasiopenda mwanga,wasiozifahamu njia za mwanga,na hawapendi kuzishika njia zake.

Kusoma sura kamili Yobu 24