Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 24:2-9 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Watu wanaoondoa alama za mipaka ya mashamba,na wengine huiba mifugo na kuilisha.

3. Huwanyanganya yatima punda wao,humweka rehani ng'ombe wa mjane.

4. Huwasukuma maskini kando ya barabara;maskini wa dunia hujificha mbele yao.

5. Kwa hiyo kama pundamwitumaskini hutafuta chakula jangwaniwapate chochote cha kuwalisha watoto wao.

6. Maskini wanalazimika kuokota mabaki ya mavuno mashambani,wanaokota katika mashamba ya mizabibu ya waovu.

7. Usiku kucha hulala uchi bila nguowakati wa baridi hawana cha kujifunikia.

8. Wamelowa kwa mvua ya milimani,hujibanza miambani kujificha wasilowe.

9. Wapo na wanaowanyakua watoto yatima vifuani mwa mama yao.Wengine huwaweka rehani watoto wa maskini.

Kusoma sura kamili Yobu 24