Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 24:14-25 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Mwuaji huamka mapema alfajiri,ili kwenda kuwaua maskini na fukara,na usiku ukifika, kazi yake ni kuiba.

15. Mzinifu naye hungojea giza liingie;akisema, ‘Hakuna atakayeniona;’kisha huuficha uso wake kwa nguo.

16. Usiku wezi huvunja nyumba,lakini mchana hujifungia ndani;wala hawajui kabisa mwanga ni nini.

17. Kwao wote giza nene ni mwanga wa asubuhi;wao ni marafiki wa vitisho vya giza nene.

18. “Lakini mwasema:‘Waovu huchukuliwa haraka na mafuriko ya maji,makao yao hubaki kuwa nchi iliyolaaniwa;hakuna aendaye kwenye mashamba yao ya mizabibu.’

19. Kama theluji inavyoyeyuka katika joto na ukamendivyo Kuzimu kunavyowanyakua waovu.

20. Maana mzazi wao huwasahau watu hao,hakuna atakayewakumbuka tena.Ndivyo uovu ulivyovunjwa kama mti.

21. “Waovu huwadhulumu wanawake wasiopata watoto.Wala hawawatendei wema wanawake wajane.

22. Mungu, kwa nguvu yake huwaangamiza wenye uwezo,huinuka nao hukata tamaa ya kuishi.

23. Huwaacha waovu wajione salama,lakini macho yake huchunguza mienendo yao.

24. Waovu hufana kwa muda tu, kisha hutoweka,hunyauka na kufifia kama jani,hukatiliwa mbali kama masuke ya ngano.

25. Nani basi, awezaye kuhakikisha kuwa mimi ni mwongona kuonesha kwamba maneno yangu si kweli?”

Kusoma sura kamili Yobu 24