Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 22:23-30 Biblia Habari Njema (BHN)

23. Ukimrudia Mungu na kunyenyekea,ukiondoa uovu mbali na makao yako,

24. ukitupilia mbali mali yako,ukaitupa dhahabu ya Ofiri ukingoni mwa kijito,

25. Mungu Mwenye Nguvu akawa ndio dhahabu yako,na fedha yako ya thamani;

26. basi, ndipo utakapomfurahia Mungu mwenye nguvuna kutazama kwa matumaini;

27. utamwomba naye atakusikiliza,nawe utazitimiza nadhiri zako.

28. Chochote utakachoamua kitafanikiwa,na mwanga utaziangazia njia zako.

29. Maana, Mungu huwaporomosha wenye majivuno,lakini huwaokoa wanyenyekevu.

30. Yeye humwokoa mtu asiye na hatia;wewe utaokolewa kwa matendo yako mema.”

Kusoma sura kamili Yobu 22