Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 22:19-27 Biblia Habari Njema (BHN)

19. Wanyofu huona na kufurahi,wasio na hatia huwacheka na kuwadharau,

20. Wanasema ama kweli maadui zetu wameangamizwa,na walichobakiza kimeteketezwa kwa moto.

21. “Sasa, Yobu, kubaliana na Mungu uwe na amani,na hapo mema yatakujia.

22. Pokea mafundisho kutoka kwake;na yaweke maneno yake moyoni mwako.

23. Ukimrudia Mungu na kunyenyekea,ukiondoa uovu mbali na makao yako,

24. ukitupilia mbali mali yako,ukaitupa dhahabu ya Ofiri ukingoni mwa kijito,

25. Mungu Mwenye Nguvu akawa ndio dhahabu yako,na fedha yako ya thamani;

26. basi, ndipo utakapomfurahia Mungu mwenye nguvuna kutazama kwa matumaini;

27. utamwomba naye atakusikiliza,nawe utazitimiza nadhiri zako.

Kusoma sura kamili Yobu 22