7. lakini atatupiliwa mbali kama mavi yake.Waliopata kumjua watajiuliza: ‘Yuko wapi?’
8. Atatoweka kama ndoto, asionekane tena,atafutika kama maono ya usiku.
9. Aliyemwona, hatamwona tena,wala pale alipoishi hapatatambuliwa tena.
10. Yeye mwenyewe itambidi kurudisha mali yake yote,watoto wake wataomba huruma kwa maskini.
11. Japo alijisikia amejaa nguvu za ujana,lakini zote zitalala pamoja naye mavumbini.
12. “Mdomoni mwake uovu ni mtamu kama sukari,anauficha chini ya ulimi wake;
13. hataki kabisa kuuachilia,bali anaushikilia kinywani mwake.
14. Lakini ufikapo tumboni huwa mchungu,mkali kama sumu ya nyoka.