Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 20:5-14 Biblia Habari Njema (BHN)

5. mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu,furaha yake asiyemcha Mungu ni ya muda mfupi tu!

6. Mwovu aweza kufana hata kufikia mbingu,kichwa chake kikafika kwenye mawingu,

7. lakini atatupiliwa mbali kama mavi yake.Waliopata kumjua watajiuliza: ‘Yuko wapi?’

8. Atatoweka kama ndoto, asionekane tena,atafutika kama maono ya usiku.

9. Aliyemwona, hatamwona tena,wala pale alipoishi hapatatambuliwa tena.

10. Yeye mwenyewe itambidi kurudisha mali yake yote,watoto wake wataomba huruma kwa maskini.

11. Japo alijisikia amejaa nguvu za ujana,lakini zote zitalala pamoja naye mavumbini.

12. “Mdomoni mwake uovu ni mtamu kama sukari,anauficha chini ya ulimi wake;

13. hataki kabisa kuuachilia,bali anaushikilia kinywani mwake.

14. Lakini ufikapo tumboni huwa mchungu,mkali kama sumu ya nyoka.

Kusoma sura kamili Yobu 20