Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 20:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Sofari, Mnaamathi, akajibu:

2. “Fikira zangu zanifanya nikujibu,wala siwezi kujizuia tena.

3. Nasikia maonyo nisiyoweza kuvumilia,lakini akili yangu yanisukuma nijibu.

4. “Wewe labda umesahau jambo hili:Kwamba tangu zamani Mungu alipomuumba mtu duniani,

5. mwovu atajiona ameshinda kwa muda tu,furaha yake asiyemcha Mungu ni ya muda mfupi tu!

6. Mwovu aweza kufana hata kufikia mbingu,kichwa chake kikafika kwenye mawingu,

7. lakini atatupiliwa mbali kama mavi yake.Waliopata kumjua watajiuliza: ‘Yuko wapi?’

8. Atatoweka kama ndoto, asionekane tena,atafutika kama maono ya usiku.

Kusoma sura kamili Yobu 20