6. Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,na kuninasa katika wavu wake.
7. Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’Lakini sijibiwi.Naita kwa sauti kubwa,lakini sipati haki yangu.
8. Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipiteamezitia giza njia zangu.
9. Amenivua fahari yangu;ameiondoa taji yangu kichwani.
10. Amenivunja pande zote, nami nimekwisha;tumaini langu amelingoa kama mti.
11. Ameichochea ghadhabu yake dhidi yangu;ameniona kuwa kama adui yake.
12. Majeshi yake yanijia kwa pamoja;yametengeneza njia ya kuja kwangu,yamepiga kambi kuizunguka nyumba yangu.
13. Mungu amewaweka ndugu zangu mbali nami;rafiki zangu wakuu wamenitoroka kabisa.