Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 19:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kisha Yobu akajibu:

2. “Mtaendelea kunitesa mpaka lini,na kunivunjavunja kwa maneno?

3. Mara hizi zote kumi mmenishutumu.Je, hamwoni aibu kunitendea vibaya?

4. Hata kama ingekuwa nimekosa kweli,kosa langu lanihusu mimi mwenyewe.

5. Mnaishusha hadhi yangu mpate kujikuza;mnanilaumu kwa kunyenyekezwa kwangu.

6. Jueni kwamba Mungu amenitendea vibaya,na kuninasa katika wavu wake.

7. Tazama napiga yowe: ‘Dhuluma!’Lakini sijibiwi.Naita kwa sauti kubwa,lakini sipati haki yangu.

8. Njia yangu ameiziba kwa ukuta ili nisipiteamezitia giza njia zangu.

Kusoma sura kamili Yobu 19