4. Wewe unajirarua mwenyewe kwa hasira zako.Kwani, dunia itaachwa tupu kwa ajili yakoau miamba ihamishwe toka mahali pake?
5. “Naam, mwanga wa mtu mwovu utazimishwa;mwali wa moto wake hautangaa.
6. Nyumbani kwake mwanga ni giza,taa inayomwangazia itazimwa.
7. Hatua zake ndefu zitafupishwa;mipango yake itamwangusha chini.
8. Nyayo zake mwenyewe zitamtia mtegoni;kila akitembea anakumbana na shimo.
9. Mtego humkamata kisiginoni,tanzi humbana kabisa.
10. Amefichiwa kitanzi ardhini;ametegewa mtego njiani mwake.
11. Hofu kuu humtisha kila upande,humfuata katika kila hatua yake.
12. Alikuwa na nguvu, lakini sasa njaa imembana;maafa yako tayari kumwangusha.