14. Anangolewa katika nyumba aliyoitegemea,na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.
15. Nyumba yake tupu, wengine wataishi humo;madini ya kiberiti yametawanywa katika makao yake.
16. Yeye ni kama mti uliokauka mizizi,matawi yake juu yamenyauka.
17. Nchini hakuna atakayemkumbuka;jina lake halitatamkwa tena barabarani.
18. Ameondolewa mwangani akatupwa gizani;amefukuzwa mbali kutoka duniani.
19. Hana watoto wala wajukuu;hakuna aliyesalia katika makao yake.
20. Watu wa magharibi wameshangazwa na yaliyompata,hofu imewakumba watu wa mashariki.
21. Hayo ndio yanayowapata wasiomjali Mungu;hapo ndipo mahali pa wasiomjua Mungu.”