Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 18:14-21 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Anangolewa katika nyumba aliyoitegemea,na kupelekwa kwa mfalme wa vitisho.

15. Nyumba yake tupu, wengine wataishi humo;madini ya kiberiti yametawanywa katika makao yake.

16. Yeye ni kama mti uliokauka mizizi,matawi yake juu yamenyauka.

17. Nchini hakuna atakayemkumbuka;jina lake halitatamkwa tena barabarani.

18. Ameondolewa mwangani akatupwa gizani;amefukuzwa mbali kutoka duniani.

19. Hana watoto wala wajukuu;hakuna aliyesalia katika makao yake.

20. Watu wa magharibi wameshangazwa na yaliyompata,hofu imewakumba watu wa mashariki.

21. Hayo ndio yanayowapata wasiomjali Mungu;hapo ndipo mahali pa wasiomjua Mungu.”

Kusoma sura kamili Yobu 18