Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 17:9-16 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Hata hivyo, mnyofu hushikilia msimamo wake,mtu atendaye mema huzidi kuwa na nguvu zaidi.

10. Lakini nyinyi njoni, njoni nyote tena,kwenu sitampata mwenye hekima hata mmoja.

11. “Siku zangu zimekwisha, mipango yangu imevunjwa;matazamio ya moyo wangu yametoweka.

12. Kwa hao rafiki zangu usiku ni mchana;je, ndio kusema mna mwanga gizani humu?

13. Kwa vile Kuzimu ndio nyumba yangu,na makao yangu yamo humo gizani;

14. kama naliita kaburi ‘baba yangu’na buu, ‘mama yangu’ au ‘dada yangu’,

15. je, nimebakiwa na tumaini gani?Ni nani awezaye kuona tumaini hilo?

16. Tazamio langu litashuka nami kuzimu!Tutateremka sote wawili hadi huko mavumbini!”

Kusoma sura kamili Yobu 17