Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 16:7-14 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Kweli Mungu amenichakazaameharibu kila kitu karibu nami.

8. Amenifanya ninyauke, na huo ni ushindi dhidi yangu.Kukonda kwangu kumenikabilina kushuhudia dhidi yangu.

9. Amenirarua kwa hasira na kunichukia;amenisagia meno;na adui yangu ananikodolea macho.

10. Watu wananidhihaki na kunicheka;makundi kwa makundi hunizunguka,na kunipiga makofi mashavuni.

11. Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,na kunitupa mikononi mwa waovu.

12. Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,

13. akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.

14. Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.

Kusoma sura kamili Yobu 16