Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 16:6-16 Biblia Habari Njema (BHN)

6. “Lakini nikisema maumivu yangu hayatulii,na nikikaa kimya hayaondoki.

7. Kweli Mungu amenichakazaameharibu kila kitu karibu nami.

8. Amenifanya ninyauke, na huo ni ushindi dhidi yangu.Kukonda kwangu kumenikabilina kushuhudia dhidi yangu.

9. Amenirarua kwa hasira na kunichukia;amenisagia meno;na adui yangu ananikodolea macho.

10. Watu wananidhihaki na kunicheka;makundi kwa makundi hunizunguka,na kunipiga makofi mashavuni.

11. Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,na kunitupa mikononi mwa waovu.

12. Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,

13. akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.

14. Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.

15. “Nimejishonea mavazi ya gunia,fahari yangu nimeibwaga mavumbini.

16. Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;

Kusoma sura kamili Yobu 16