Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 16:12-17 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,

13. akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.

14. Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.

15. “Nimejishonea mavazi ya gunia,fahari yangu nimeibwaga mavumbini.

16. Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;

17. ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,na sala zangu kwa Mungu ni safi.

Kusoma sura kamili Yobu 16