Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 16:11-21 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Mungu amenitia mikononi mwa wajeuri,na kunitupa mikononi mwa waovu.

12. Nilikuwa nimestarehe, lakini akanivunjavunja,alinikaba shingo na kunipasua vipandevipande;alinifanya shabaha ya mishale yake,

13. akanipiga mishale kutoka kila upande.Amenipasua figo bila huruma,na nyongo yangu akaimwaga chini.

14. Hunivunja na kunipiga tena na tena;hunishambulia kama askari.

15. “Nimejishonea mavazi ya gunia,fahari yangu nimeibwaga mavumbini.

16. Uso wangu ni mwekundu kwa kulia,kope zangu zimekuwa nyeusi ti;

17. ingawa sijafanya dhuluma kwa mkono wangu,na sala zangu kwa Mungu ni safi.

18. “Ewe dunia, usiifunike damu yangu iliyomwagika;kilio changu kienee kila mahali.

19. Nina hakika ninaye shahidi wangu mbinguni,mwenye kunitetea yuko huko juu.

20. Rafiki zangu wanidharau;nabubujika machozi kumwomba Mungu.

21. Laiti mtu angenitetea mbele ya Mungu,kama ifanyikavyo duniani kati za watu wawili.

Kusoma sura kamili Yobu 16