Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 15:4-9 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Lakini wewe unapuuza uchaji wa Mungu;na kuzuia kutafakari mbele ya Mungu.

5. Uovu wako ndio unaokifundisha kinywa chako,nawe wachagua kusema kama wadanganyifu.

6. Maneno yako mwenyewe yanakuhukumu, sio mimi;matamshi yako yashuhudia dhidi yako.

7. Je, wewe ni mtu wa kwanza kuzaliwa?Je, wewe ulizaliwa kabla ya kuweko vilima?

8. Je, ulipata kuweko katika halmashauri ya Mungu?au, wewe ndiwe peke yako mwenye hekima?

9. Unajua kitu gani tusichokijua sisi?Unafahamu kitu gani tusichokifahamu sisi?

Kusoma sura kamili Yobu 15