Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 15:22-28 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Mwovu hana tumaini la kutoka gizani;mwisho wake ni kufa kwa upanga.

23. Hutangatanga kutafuta chakula,akisema, ‘Kiko wapi?’Ajua kwamba siku ya giza inamkaribia.

24. Taabu na uchungu, vyamtisha;vyamkabili kama jeshi la mfalme anayeshambulia.

25. Kwa sababu amenyosha mkono wake dhidi ya Mungu;akadiriki kumpinga huyo Mungu mwenye nguvu;

26. alikimbia kwa kiburi kumshambulia,huku ana ngao yenye mafundo makubwa.

27. Uso wake ameunenepesha kwa mafuta,na kiuno chake kimejaa mafuta.

28. Ameishi katika miji iliyoachwa tupu,katika nyumba zisizokaliwa na mtu;nyumba zilizotakiwa ziwe lundo la uharibifu.

Kusoma sura kamili Yobu 15