Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 15:20-26 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Mwovu atateseka kwa maumivu siku zote,miaka yote waliyopangiwa wakatili.

21. Sauti za vitisho zitampigia kelele masikioni,anapodhani amestawi mwangamizi atamvamia.

22. Mwovu hana tumaini la kutoka gizani;mwisho wake ni kufa kwa upanga.

23. Hutangatanga kutafuta chakula,akisema, ‘Kiko wapi?’Ajua kwamba siku ya giza inamkaribia.

24. Taabu na uchungu, vyamtisha;vyamkabili kama jeshi la mfalme anayeshambulia.

25. Kwa sababu amenyosha mkono wake dhidi ya Mungu;akadiriki kumpinga huyo Mungu mwenye nguvu;

26. alikimbia kwa kiburi kumshambulia,huku ana ngao yenye mafundo makubwa.

Kusoma sura kamili Yobu 15