20. Mwovu atateseka kwa maumivu siku zote,miaka yote waliyopangiwa wakatili.
21. Sauti za vitisho zitampigia kelele masikioni,anapodhani amestawi mwangamizi atamvamia.
22. Mwovu hana tumaini la kutoka gizani;mwisho wake ni kufa kwa upanga.
23. Hutangatanga kutafuta chakula,akisema, ‘Kiko wapi?’Ajua kwamba siku ya giza inamkaribia.
24. Taabu na uchungu, vyamtisha;vyamkabili kama jeshi la mfalme anayeshambulia.
25. Kwa sababu amenyosha mkono wake dhidi ya Mungu;akadiriki kumpinga huyo Mungu mwenye nguvu;
26. alikimbia kwa kiburi kumshambulia,huku ana ngao yenye mafundo makubwa.