Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 15:15-21 Biblia Habari Njema (BHN)

15. Ikiwa Mungu hawaamini hata watakatifu wake,nazo mbingu si safi mbele yake,

16. sembuse binadamu aliye kinyaa na mpotovubinadamu atendaye uovu kama kunywa maji!

17. “Sasa nisikilize, nami nitakuonesha,nitakuambia yale niliyoyaona,

18. mafundisho ya wenye hekima,mambo ambayo wazee wao hawakuyaficha,

19. ambao Mungu aliwapa hiyo nchi peke yao,wala hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao.

20. Mwovu atateseka kwa maumivu siku zote,miaka yote waliyopangiwa wakatili.

21. Sauti za vitisho zitampigia kelele masikioni,anapodhani amestawi mwangamizi atamvamia.

Kusoma sura kamili Yobu 15