Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 15:11-23 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Je, faraja anazokupa Mungu ni ndogo mno?Au je, neno lake la upole kwako si kitu?

12. Mbona moyo unakusukuma kukasirikana kutoa macho makali,

13. hata kumwasi Munguna kusema maneno mabaya kama hayo?

14. Mtu ni nini hata aweze kuwa mwadilifu?au yule aliyezaliwa na mwanamke hata aweze kuwa mwema?

15. Ikiwa Mungu hawaamini hata watakatifu wake,nazo mbingu si safi mbele yake,

16. sembuse binadamu aliye kinyaa na mpotovubinadamu atendaye uovu kama kunywa maji!

17. “Sasa nisikilize, nami nitakuonesha,nitakuambia yale niliyoyaona,

18. mafundisho ya wenye hekima,mambo ambayo wazee wao hawakuyaficha,

19. ambao Mungu aliwapa hiyo nchi peke yao,wala hakuna mgeni aliyepita miongoni mwao.

20. Mwovu atateseka kwa maumivu siku zote,miaka yote waliyopangiwa wakatili.

21. Sauti za vitisho zitampigia kelele masikioni,anapodhani amestawi mwangamizi atamvamia.

22. Mwovu hana tumaini la kutoka gizani;mwisho wake ni kufa kwa upanga.

23. Hutangatanga kutafuta chakula,akisema, ‘Kiko wapi?’Ajua kwamba siku ya giza inamkaribia.

Kusoma sura kamili Yobu 15