Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 14:3-15 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Ee Mungu, kwa nini unajali hata kumwangaliana kuanza kuhojiana naye?

4. Nani awezaye kutoa kitu kisafi kutoka kitu kichafu?Hakuna anayeweza.

5. Siku za kuishi binadamu zimepimwa;ee, Mungu umeipanga idadi ya miezi yake;hawezi kupita kikomo ulichomwekea.

6. Angalia pembeni basi, umwache;ili apate kufurahia siku zake kama kibarua.

7. Maana mti ukikatwa lipo tumaini la kuota,waweza kuchipua tena.

8. Japo mizizi yake itazeeka udongoni,na shina lake kufia ardhini,

9. lakini kwa harufu tu ya maji utachipua;utatoa matawi kama chipukizi.

10. Lakini mtu hufa na huo ndio mwisho wake.Akisha toa roho anabakiwa na nini tena?

11. “Kama vile maji yakaukavyo ziwani,na mto unavyokoma kutiririka,

12. ndivyo anavyokufa mtu, wala haamki tena;hataamka tena wala kugutuka,hata hapo mbingu zitakapotoweka.

13. “Laiti ungenificha kuzimu;ungenificha hadi ghadhabu yako ipoe;nao muda ulionipimia ukiisha ungenikumbuka.

14. Je, mtu akifa anaweza kuishi tena?Siku zangu zote za kazi ningekungojahadi wakati wa kufunguliwa ufike.

15. Hapo ungeniita, nami ningeitika,wakati ungetaka kuniona mimi kiumbe chako.

Kusoma sura kamili Yobu 14