Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 13:3-9 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Lakini ningependa kusema na Mungu mwenye nguvu,natamani kujitetea mbele zake Mungu.

4. Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa;nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.

5. Laiti mngekaa kimya kabisa,ikafikiriwa kwamba mna hekima!

6. Sikilizeni basi hoja yangu,nisikilizeni ninapojitetea.

7. Je, mnadhani mwamtumikia Mungu kwa kusema uongo?Mnafikiri kusema kwa hila kunamfaa yeye?

8. Je, mnajaribu kumpendelea Mungu?Je, mtamtetea Mungu mahakamani?

9. Je, akiwakagua nyinyi mtapona?Au mnadhani mnaweza kumdanganya Mungu kama watu?

Kusoma sura kamili Yobu 13