Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 13:13-22 Biblia Habari Njema (BHN)

13. “Nyamazeni, nami niongee.Yanipate yatakayonipata.

14. Niko tayari hata kuhatarishamaisha yangu;

15. Mungu aniue akitaka, sina la kupoteza,hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.

16. Kama nikifaulu hapo nitakuwa nimeshinda,maana mtu mwovu hawezi kwenda mbele yake.

17. Sikilizeni kwa makini maneno yangu,maelezo yangu na yatue masikioni mwenu.

18. Kesi yangu nimeiandaa vilivyo,nina hakika mimi sina hatia.

19. “Nani atakayeipinga hoja yangu?Niko tayari kunyamaza na kufa.

20. Mungu wangu, nijalie tu haya mawili,nami sitajificha mbali na wewe:

21. Kwanza uniondolee mkono wako unaonipiga,na usiniangamize kwa kitisho chako.

22. “Uanze kutoa hoja yako nami nikujibu.Au mimi nianze, nawe unijibu.

Kusoma sura kamili Yobu 13