Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 13:10-19 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Hakika yeye atawakemeakama mkionesha upendeleo kwa siri.

11. Je, fahari yake haiwatishi?Je, hampatwi na hofu juu yake?

12. Misemo yenu ni methali za majivu,hoja zenu ni ngome za udongo.

13. “Nyamazeni, nami niongee.Yanipate yatakayonipata.

14. Niko tayari hata kuhatarishamaisha yangu;

15. Mungu aniue akitaka, sina la kupoteza,hata hivyo nitautetea mwenendo wangu mbele yake.

16. Kama nikifaulu hapo nitakuwa nimeshinda,maana mtu mwovu hawezi kwenda mbele yake.

17. Sikilizeni kwa makini maneno yangu,maelezo yangu na yatue masikioni mwenu.

18. Kesi yangu nimeiandaa vilivyo,nina hakika mimi sina hatia.

19. “Nani atakayeipinga hoja yangu?Niko tayari kunyamaza na kufa.

Kusoma sura kamili Yobu 13