Agano la Kale

Agano Jipya

Yobu 13:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Tazama, hayo yote nimeyaona kwa macho yangu;nimeyasikia kwa masikio yangu mwenyewe na kuelewa.

2. Yote mnayoyajua, mimi pia nayajua.Mimi si mtu duni kuliko nyinyi.

3. Lakini ningependa kusema na Mungu mwenye nguvu,natamani kujitetea mbele zake Mungu.

4. Lakini nyinyi mnaupakaa uongo chokaa;nyinyi nyote ni waganga wasiofaa kitu.

5. Laiti mngekaa kimya kabisa,ikafikiriwa kwamba mna hekima!

6. Sikilizeni basi hoja yangu,nisikilizeni ninapojitetea.

7. Je, mnadhani mwamtumikia Mungu kwa kusema uongo?Mnafikiri kusema kwa hila kunamfaa yeye?

8. Je, mnajaribu kumpendelea Mungu?Je, mtamtetea Mungu mahakamani?

Kusoma sura kamili Yobu 13