Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 9:6-14 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Wanarundika dhuluma juu ya dhuluma,na udanganyifu juu ya udanganyifu.Wanakataa kunitambua mimi.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

7. Kwa hiyo mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi nasema:Tazama, nitawayeyusha na kuwajaribu!Au, nifanye nini zaidi na watu wangu waovu?

8. Ndimi zao ni kama mishale yenye sumu,daima haziishi kudanganya;kila mmoja huongea vema na jirani yake,lakini moyoni mwake hupanga kumshambulia.

9. Je, nisiwaadhibu kwa sababu ya mambo haya?Je, nisilipe kisasi kwa taifa kama hili?Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

10. Nitaililia na kuiomboleza milima;nitayaombolezea malisho nyikani,kwa sababu yamekauka kabisa,hakuna mtu apitaye mahali hapo.Hakusikiki tena sauti za ng'ombe;ndege na wanyama wamekimbia na kutoweka.

11. Mwenyezi-Mungu asema:“Nitaifanya Yerusalemu magofu matupu,naam, nitaifanya kuwa pango la mbweha;na miji ya Yuda nitaifanya kuwa jangwa,mahali pasipokaliwa na mtu yeyote.”

12. Nami nikauliza, “Je kuna mtu mwenye hekima kiasi cha kuweza kueleza mambo haya? Mwenyezi-Mungu aliongea na nani hata huyo aweze kutangaza kitu hicho? Kwa nini nchi imeharibiwa na kufanywa tupu kama jangwa hata hakuna mtu apitaye humo?”

13. Mwenyezi-Mungu akajibu: “Kwa kuwa wamekataa kushika sheria yangu niliyowapa, wamekataa kutii sauti yangu na kufuata matakwa yake.

14. Badala yake wamefuata kwa ukaidi fikira za mioyo yao, wakaenda kuyaabudu Mabaali kama walivyofundishwa na wazee wao.

Kusoma sura kamili Yeremia 9