Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 9:13-26 Biblia Habari Njema (BHN)

13. Mwenyezi-Mungu akajibu: “Kwa kuwa wamekataa kushika sheria yangu niliyowapa, wamekataa kutii sauti yangu na kufuata matakwa yake.

14. Badala yake wamefuata kwa ukaidi fikira za mioyo yao, wakaenda kuyaabudu Mabaali kama walivyofundishwa na wazee wao.

15. Basi, mimi Mwenyezi-Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, nasema hivi: Tazama nitawalisha watu hawa uchungu na kuwapa maji yenye sumu wanywe.

16. Nitawatawanya kati ya mataifa ambayo wao wenyewe wala wazee wao hawakupata kuyajua; nitawafanya waandamwe na vita mpaka hapo nitakapowaangamiza wote.”

17. Mwenyezi-Mungu wa majeshi asema hivi:“Fikirini na kuwaita wanawake waomboleze;naam, waiteni wanawake hodari wa kuomboleza.

18. Waambieni: ‘Njoni hima mkaomboleze juu yetu,macho yetu yapate kuchuruzika machozi,na kope zetu zibubujike machozi kama maji.’”

19. Kilio kinasikika Siyoni:“Tumeangamia kabisa!Tumeaibishwa kabisa!Lazima tuiache nchi yetu,maana nyumba zetu zimebomolewa!

20. Enyi wanawake, sikilizeni neno la Mwenyezi-Mungu!Tegeni masikio msikie jambo analosema.Wafundisheni binti zenu kuomboleza,na jirani zenu wimbo wa maziko:

21. ‘Kifo kimepenya madirisha yetu,kimeingia ndani ya majumba yetu;kimewakatilia mbali watoto wetu barabarani,vijana wetu katika viwanja vya mji.

22. Maiti za watu zimetapakaa kila mahalikama marundo ya mavi mashambani,kama masuke yaliyoachwa na mvunaji,wala hakuna atakayeyakusanya.’Ndivyo alivyoniambia Mwenyezi-Mungu niseme.”

23. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Mwenye hekima asijivunie nguvu zake,wala tajiri asijivunie utajiri wake.

24. Anayetaka kujivuna na ajivunie jambo hili:Kwamba ananifahamukwamba anajua Mwenyezi-Mungu hutenda mema,hufanya mambo ya haki na uadilifu duniani.Watu wa namna hiyo ndio wanipendezao.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

25. Mwenyezi-Mungu asema: “Siku zaja ambapo nitawaadhibu wote waliotahiriwa mwilini tu:

26. Wamisri, Wayuda, Waedomu, Waamoni, Wamoabu na wakazi wote wa jangwani wanaonyoa denge. Maana watu hawa wote na Waisraeli wote hawakutahiriwa moyoni.”

Kusoma sura kamili Yeremia 9