Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:41-48 Biblia Habari Njema (BHN)

41. Ajabu kutekwa kwa Babuloni;mji uliosifika duniani kote umechukuliwa!Babuloni umekuwa kinyaa kati ya mataifa!

42. Bahari imefurika juu ya Babuloni,Babuloni imefunikwa mawimbi yaliyochafuka.

43. Miji yake imekuwa kinyaa,nchi ya ukavu na jangwa,nchi isiyokaliwa na mtu yeyote,wala kupitika na binadamu yeyote.

44. Nitamwadhibu mungu Beli huko Babuloni,nitamfanya akitoe alichokimeza.Mataifa hayatamiminika tena kumwendea.Ukuta wa Babuloni umebomoka.

45. “Tokeni humo enyi watu wangu!Kila mtu na ayasalimishe maisha yake,kutoka hasira kali ya Mwenyezi-Mungu.

46. Msife moyo wala msiwe na hofu,kwa sababu ya uvumi mnaosikia nchini.Mwaka huu kuna uvumi huu,mwaka mwingine uvumi mwingine;uvumi wa ukatili katika nchi,mtawala mmoja dhidi ya mtawala mwingine.

47. Kweli siku zaja,nitakapoadhibu sanamu za Babuloni;nchi yake yote itatiwa aibu,watu wake wote watauawa humohumo.

48. Kisha mbingu, dunia na vyote vilivyomovitaimba kwa furaha kuhusu kuanguka kwa Babuloni,waangamizi watakapofika kutoka kaskazini kuushambulia.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Kusoma sura kamili Yeremia 51