Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:35-44 Biblia Habari Njema (BHN)

35. Watu wa Yerusalemu na waseme:“Babuloni na ulipizwe ukatili uleule,tuliotendwa sisi pamoja na jamaa zetu!Babuloni ipatilizwekwa umwagaji wa damu yetu.”

36. Kwa hiyo asema hivi Mwenyezi-Mungu:“Nitawatetea kuhusu kisa chenu,na kulipiza kisasi kwa ajili yenu.Nitaikausha bahari ya Babulonina kuvifanya visima vyake vikauke.

37. Babuloni itakuwa rundo la magofu,itakuwa makao ya mbweha,itakuwa kinyaa na kitu cha kuzomewa;hakuna mtu atakayekaa huko.

38. Wababuloni watanguruma pamoja kama simba;watakoroma kama wanasimba.

39. Wakiwa na uchu mkubwanitawaandalia karamu:Nitawalewesha mpaka wapepesuke;nao watalala usingizi wa daimana hawataamka tena.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

40. Nitawashusha chini kama kondoo wa kuchinjwa,kama vile kondoo dume na beberu.

41. Ajabu kutekwa kwa Babuloni;mji uliosifika duniani kote umechukuliwa!Babuloni umekuwa kinyaa kati ya mataifa!

42. Bahari imefurika juu ya Babuloni,Babuloni imefunikwa mawimbi yaliyochafuka.

43. Miji yake imekuwa kinyaa,nchi ya ukavu na jangwa,nchi isiyokaliwa na mtu yeyote,wala kupitika na binadamu yeyote.

44. Nitamwadhibu mungu Beli huko Babuloni,nitamfanya akitoe alichokimeza.Mataifa hayatamiminika tena kumwendea.Ukuta wa Babuloni umebomoka.

Kusoma sura kamili Yeremia 51