Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:33-36 Biblia Habari Njema (BHN)

33. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema hivi:“Babuloni ni kama uwanja wa kupuria nafakawakati unapotayarishwa.Lakini bado kidogo tu,wakati wa mavuno utaufikia.”

34. Mfalme Nebukadneza wa Babulonialiuharibu na kuuponda mji wa Yerusalemualiuacha kama chungu kitupu;aliumeza kama joka.Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri,akautupilia mbali kama matapishi.

35. Watu wa Yerusalemu na waseme:“Babuloni na ulipizwe ukatili uleule,tuliotendwa sisi pamoja na jamaa zetu!Babuloni ipatilizwekwa umwagaji wa damu yetu.”

36. Kwa hiyo asema hivi Mwenyezi-Mungu:“Nitawatetea kuhusu kisa chenu,na kulipiza kisasi kwa ajili yenu.Nitaikausha bahari ya Babulonina kuvifanya visima vyake vikauke.

Kusoma sura kamili Yeremia 51