Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:27-41 Biblia Habari Njema (BHN)

27. Tweka bendera ya vita duniani,piga tarumbeta kati ya mataifa;yatayarishe mataifa kupigana naye;ziite falme kuishambulia;falme za Ararati, Mini na Ashkenazi.Weka majemadari dhidi yake;walete farasi kama makundi ya nzige.

28. Yatayarishe mataifa kupigana naye vita;watayarishe wafalme wa Medi, watawala na mawakili wao,tayarisheni nchi zote katika himaya yake.

29. Nchi inatetemeka na kugaagaa kwa maumivu,maana nia ya Mwenyezi-Mungu kuhusu Babuloni ni thabiti:Ataifanya nchi ya Babuloni kuwa jangwa,ataifanya iwe bila watu.

30. Askari wa Babuloni wameshindwa kupigana,wamebaki katika ngome zao;nguvu zao zimewaishia,wamekuwa kama wanawake.Nyumba za Babuloni zimechomwa moto,malango yake ya chuma yamevunjwa.

31. Tarishi baada ya tarishi wanapiga mbio,mjumbe mmoja anamfuata mjumbe mwingine,kumpasha habari mfalme wa Babulonikwamba mji wake umevamiwa kila upande.

32. Vivuko vya mto vimetekwa,ngome zimechomwa moto,askari wamekumbwa na hofu.

33. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema hivi:“Babuloni ni kama uwanja wa kupuria nafakawakati unapotayarishwa.Lakini bado kidogo tu,wakati wa mavuno utaufikia.”

34. Mfalme Nebukadneza wa Babulonialiuharibu na kuuponda mji wa Yerusalemualiuacha kama chungu kitupu;aliumeza kama joka.Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri,akautupilia mbali kama matapishi.

35. Watu wa Yerusalemu na waseme:“Babuloni na ulipizwe ukatili uleule,tuliotendwa sisi pamoja na jamaa zetu!Babuloni ipatilizwekwa umwagaji wa damu yetu.”

36. Kwa hiyo asema hivi Mwenyezi-Mungu:“Nitawatetea kuhusu kisa chenu,na kulipiza kisasi kwa ajili yenu.Nitaikausha bahari ya Babulonina kuvifanya visima vyake vikauke.

37. Babuloni itakuwa rundo la magofu,itakuwa makao ya mbweha,itakuwa kinyaa na kitu cha kuzomewa;hakuna mtu atakayekaa huko.

38. Wababuloni watanguruma pamoja kama simba;watakoroma kama wanasimba.

39. Wakiwa na uchu mkubwanitawaandalia karamu:Nitawalewesha mpaka wapepesuke;nao watalala usingizi wa daimana hawataamka tena.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

40. Nitawashusha chini kama kondoo wa kuchinjwa,kama vile kondoo dume na beberu.

41. Ajabu kutekwa kwa Babuloni;mji uliosifika duniani kote umechukuliwa!Babuloni umekuwa kinyaa kati ya mataifa!

Kusoma sura kamili Yeremia 51