Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:24-35 Biblia Habari Njema (BHN)

24. “Nitaiadhibu Babuloni na wakazi wote wa Kaldayo mkiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Siyoni. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

25. Mimi ninapingana nawe ewe mlima mharibifu,mlima unaoharibu dunia nzima!Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.Nitanyosha mkono wangu dhidi yako,nitakuangusha kutoka miambani juuna kukufanya kuwa mlima uliochomwa moto;

26. hata hamna jiwe lako litakalochukuliwa kujengea,hakuna jiwe litakalochukuliwa kuwekea msingi!Utakuwa kama jangwa milele.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

27. Tweka bendera ya vita duniani,piga tarumbeta kati ya mataifa;yatayarishe mataifa kupigana naye;ziite falme kuishambulia;falme za Ararati, Mini na Ashkenazi.Weka majemadari dhidi yake;walete farasi kama makundi ya nzige.

28. Yatayarishe mataifa kupigana naye vita;watayarishe wafalme wa Medi, watawala na mawakili wao,tayarisheni nchi zote katika himaya yake.

29. Nchi inatetemeka na kugaagaa kwa maumivu,maana nia ya Mwenyezi-Mungu kuhusu Babuloni ni thabiti:Ataifanya nchi ya Babuloni kuwa jangwa,ataifanya iwe bila watu.

30. Askari wa Babuloni wameshindwa kupigana,wamebaki katika ngome zao;nguvu zao zimewaishia,wamekuwa kama wanawake.Nyumba za Babuloni zimechomwa moto,malango yake ya chuma yamevunjwa.

31. Tarishi baada ya tarishi wanapiga mbio,mjumbe mmoja anamfuata mjumbe mwingine,kumpasha habari mfalme wa Babulonikwamba mji wake umevamiwa kila upande.

32. Vivuko vya mto vimetekwa,ngome zimechomwa moto,askari wamekumbwa na hofu.

33. Mwenyezi-Mungu, Mungu wa Israeli asema hivi:“Babuloni ni kama uwanja wa kupuria nafakawakati unapotayarishwa.Lakini bado kidogo tu,wakati wa mavuno utaufikia.”

34. Mfalme Nebukadneza wa Babulonialiuharibu na kuuponda mji wa Yerusalemualiuacha kama chungu kitupu;aliumeza kama joka.Alijaza tumbo lake vitu vyake vizurivizuri,akautupilia mbali kama matapishi.

35. Watu wa Yerusalemu na waseme:“Babuloni na ulipizwe ukatili uleule,tuliotendwa sisi pamoja na jamaa zetu!Babuloni ipatilizwekwa umwagaji wa damu yetu.”

Kusoma sura kamili Yeremia 51