Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:24-30 Biblia Habari Njema (BHN)

24. “Nitaiadhibu Babuloni na wakazi wote wa Kaldayo mkiona kwa macho yenu wenyewe, kwa sababu ya uovu wote walioufanya katika Siyoni. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

25. Mimi ninapingana nawe ewe mlima mharibifu,mlima unaoharibu dunia nzima!Nasema mimi Mwenyezi-Mungu.Nitanyosha mkono wangu dhidi yako,nitakuangusha kutoka miambani juuna kukufanya kuwa mlima uliochomwa moto;

26. hata hamna jiwe lako litakalochukuliwa kujengea,hakuna jiwe litakalochukuliwa kuwekea msingi!Utakuwa kama jangwa milele.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

27. Tweka bendera ya vita duniani,piga tarumbeta kati ya mataifa;yatayarishe mataifa kupigana naye;ziite falme kuishambulia;falme za Ararati, Mini na Ashkenazi.Weka majemadari dhidi yake;walete farasi kama makundi ya nzige.

28. Yatayarishe mataifa kupigana naye vita;watayarishe wafalme wa Medi, watawala na mawakili wao,tayarisheni nchi zote katika himaya yake.

29. Nchi inatetemeka na kugaagaa kwa maumivu,maana nia ya Mwenyezi-Mungu kuhusu Babuloni ni thabiti:Ataifanya nchi ya Babuloni kuwa jangwa,ataifanya iwe bila watu.

30. Askari wa Babuloni wameshindwa kupigana,wamebaki katika ngome zao;nguvu zao zimewaishia,wamekuwa kama wanawake.Nyumba za Babuloni zimechomwa moto,malango yake ya chuma yamevunjwa.

Kusoma sura kamili Yeremia 51