Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:2-10 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Nitawapeleka wapepetaji Babuloni,nao watampepeta;watamaliza kila kitu katika nchi yakewatakapofika kuishambulia toka kila upandewakati wa maangamizi yake.”

3. Usiwape nafasi wapiga mshale wa Babuloni;usiwaache wavute upinde,wala kuvaa mavazi yao ya vita.Usiwahurumie vijana wake;liangamize kabisa jeshi lake.

4. Wataanguka na kuuawa katika nchi ya Wakaldayo,watajeruhiwa katika barabara zake.

5. Lakini Israeli na Yuda hawakuachwa na Mungu wao Mwenyezi-Mungu wa majeshi,ingawa nchi yao imejaa hatia mbele yake yeye Mtakatifu wa Israeli.

6. Kimbieni kutoka Babuloni,kila mtu na ayaokoe maisha yake!Msiangamizwe katika adhabu yake,maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipa kisasi,anaiadhibu Babuloni kama inavyostahili.

7. Babuloni ilikuwa kikombe cha dhahabumkononi mwa Mwenyezi-Mungu,ambacho kiliilewesha dunia nzima.Mataifa yalikunywa divai yake,hata yakapatwa wazimu.

8. Ghafla Babuloni imeanguka na kuvunjikavunjika;ombolezeni kwa ajili yake!Leteni dawa kutuliza maumivu yake;labda utaweza kuponywa.

9. Tulijaribu kuuponya Babuloni,lakini hauwezi kuponywa.Uacheni, twendeni zetu,kila mmoja katika nchi yake,maana hukumu yake ni kuu mnoimeinuka mpaka mawinguni.

10. Mwenyezi-Mungu amethibitisha kuwa hatuna hatia.Twendeni Siyoni tukatangazematendo ya Mwenyezi-Mungu, Mungu wetu.

Kusoma sura kamili Yeremia 51