Agano la Kale

Agano Jipya

Yeremia 51:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Nitachochea upepo wa kuangamiza dhidi ya Babuloni,dhidi ya wakazi wa Kaldayo.

2. Nitawapeleka wapepetaji Babuloni,nao watampepeta;watamaliza kila kitu katika nchi yakewatakapofika kuishambulia toka kila upandewakati wa maangamizi yake.”

3. Usiwape nafasi wapiga mshale wa Babuloni;usiwaache wavute upinde,wala kuvaa mavazi yao ya vita.Usiwahurumie vijana wake;liangamize kabisa jeshi lake.

4. Wataanguka na kuuawa katika nchi ya Wakaldayo,watajeruhiwa katika barabara zake.

5. Lakini Israeli na Yuda hawakuachwa na Mungu wao Mwenyezi-Mungu wa majeshi,ingawa nchi yao imejaa hatia mbele yake yeye Mtakatifu wa Israeli.

6. Kimbieni kutoka Babuloni,kila mtu na ayaokoe maisha yake!Msiangamizwe katika adhabu yake,maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipa kisasi,anaiadhibu Babuloni kama inavyostahili.

Kusoma sura kamili Yeremia 51